Subscribe to Updates
Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.
- EPUKA MAUA HAYA NYUMBANI KWAKO
- FUKUZA NYOKA KWA MIMEA HII
- DARASA LA SABA KUPEWA UFADHILI
- MAENDELEO BENKI YATAJA ONGEZEKO LA FAIDA 2024
- BRELA, UDSM wawanoa wadau faida miliki ubunifu
- Utafiti kilimo, mifugo na uvuvi kutokomeza njaa
- NMB yaja na mwarobaini mikopo kausha damu
- TARI kuzalisha miche 100,000 ya parachichi msimu ujao
Author: Mama Mwenyekiti
DAKIKA mbili na sekunde 14 tangu walipoanza kuonyesha ufundi wao wa kucheza muziki, watoto wa ‘mtaani’ kutoka jiji la Kampala Uganda, zilitosha kumnyanyua jaji Bruno Tonioli, ambaye aliwapa alama ya dhahabu kwa burudani waliyokuwa wanaitoa. Hawa si wengine bali ni kundi la Ghetto Kids, linalolelewa na mwalimu Dauda Kavuma, ambaye anawachukua kutoka mitaani wengine wakiwa yatima au kukosa malezi; na hivyo kuwapa malezi pamoja na huduma zote muhimu. Watoto hawa wamefanikiwa wateka mioyo ya takribani mashabiki 2,286 waliokuwa wanafuatilia onyesho la vipaji la Britain Got Talent, wakati wa kurekodiwa katika ukumbi wa Palladium, jijini London, nchini Uingereza wiki mbili zilizopita.…
DODOMA, Tanzania WAKATI watu wengi wakitazama njiwa kama kitoweo na mapambo, ndege huyo anaweza kufugwa kibiashara na kuiingizia familia kipato cha kutosha. Deogratius Temba, kijana kutoka Dodoma, Tanzania anafuga njiwa wa kipekee na wanamuingizia kipato cha kutosha. Njiwa anaofuga Temba maarufu kama Manjiwa hutumika kupendezesha makazi, maofisi ama sehemu zingine kama mahoteli na za kupumzikia. Kati zaidi ya aina 10 ya njiwa wa mapambo alionao Deogratius, mmoja anauzwa kati ya dola $85 mpaka $180 au Sh. 400,000. Unaweza kujiuliza wanafananaje njiwa hawa, na kwanini kijana huyu maarufu kama Deo Manjiwa ameamua kuwafuga njiwa hawa wa mapambo? Mwandishi wetu Yusuph Mazimu…
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega. WAFUGAJI kote nchini wametakiwa kutenga maeneo ya malisho katika msimu huu wa mvua kwa ajili ya matumizi wakati wa kiangazi, ili kuepuka migogoro baina yao na wakulima. Kamanda wa Kikosi cha Kuzuia wizi wa Mifugo nchini, ACP Simon Pasua, aliyasema hayo jana wilayani Monduli, alipokutana na viongozi wa wafugaji pamoja na wakulima, kwa lengo la kupanga mikakati ya pamoja ya kuepusha migogoro ambayo imekua ikijitokeza wakati wa kiangazi. Kamanda Pasua alibainisha kuwa wakati wa kiangazi kunakuwa na ukame hivyo kukosekana sehemu za malisho, hali ambayo inasababisha baadhi ya wafugaji kupeleka mifugo sehemu ambazo…
Mwonekano wa bwawa la kufua umeme la Julius Nyerere Na Restuta James MIEZI minne baada ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, kuzindua ujazaji wa maji katika bwawa la kufua umeme la Julius Nyerere (JNHPP), katika Mto Rufiji, mkoani Pwani, ujenzi wake umebakisha asilimia 14.4 pekee kukamilika. Bwawa hilo linalotazamiwa kuzalisha megawati 2,115 za umeme litakapokamilika, limebakisha ujazo wa maji futi 10.53 pekee, kuanza uzalishaji wa awali. Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, amewaambia waandishi wa habari leo kwamba ujenzi wa mradi huo umefikia asilimia 85.6. “Bwawa letu la Mwalimu Nyerere ni moja ya miradi ambayo inakwenda vizuri na utekelezaji unaendelea…mwakani Juni tunataka…
Mwenyekiti wa Tume ya Rais ya kuangalia namna ya kuboresha mifumo ya hakijinai nchini, Jaji Mkuu Mstaafu, Othman Mohamed Chande. Na Restuta James MALEZI duni, umasikini utandawazi na makundi rika, yanasababisha watoto kufanya makosa makubwa ya kijinai kama mauaji na kufanya unyang’anyi kwa kutumia silaha, ili kupata mahitaji muhimu. Meneja wa mahabusu ya Watoto jijini Dar es Salaam, Darius Damas, ameiambia Tume ya Kuangalia namna ya Kuboresha Mifumo ya Hakijiani inayoongozwa na Jaji Mkuu Mstaafu, Othman Mohamed Chande, ilipotembelea mahabusu hiyo leo. Amesema mashtaka yanayowakabili watoto ni mauaji, unyang’anyi wa kutumia silaha, ulawiti na ubakaji, matusi, dawa za kulevya na…
Na Restuta James UWEKEZAJI uliofanywa na Serikali ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, katika bandari ya Dar es Salaam, umeiongezea uwezo na sasa inategemea kuhudumia zaidi ya tani milioni 20 za shehena mchanganyiko kwa mwaka. Tangu Rais Samia aiingie madarakani, ameshatoa zaidi ya Sh. bilioni 573 ili kuwekeza katika Bandari ya Dar es salaam ikiwamo ununuzi wa mitambo ya kisasa ya kupakua na kupakia makontena. Ni katika uwekezaji huo ambao umewezesha bandari nzima kufungwa kamera, ili kudhibiti wizi na kuhakikisha usalama wa shehena inayohudumiwa na bandari ya Dar es Salaam. Lengo la uwekezaji huo ni kuchochea kasi na ukuaji uchumi,…
Mwandishi Wetu na Mtandao KUNA watu ambao huwezi kukadiria umri wao licha ya kwamba wana miaka mingi, mwonekano wao unabakia kuwa wa ujana. Orodha ya Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), inawataja nyota kadhaa wa muziki na filamu, ambao kwa miaka mingi wamesalia kama walivyokua walipojitosa katika fani ya burudani. Kuanzia Afrika, orodha ya BBC inamtaja mwigizaji wa Nollywood nchini Nigeria, Kate Henshaw (51), ambaye mwonekano wake haufanani na miaka aliyonayo. Mashabiki wengi wa Kate walikadiria ana miaka 30, wakati aliposherehekea miaka 50 tangu kuzaliwa kwake. Kwa ufupi ni kwamba Kate Henshaw aliolewa na raia wa Uingereza, Roderick James Nuttal, mwaka wa 1999 na wakajaaliwa mtoto wa…
Na Restuta James UTAFITI wa kitabibu umeongeza matumaini katika vita dhidi ya Virusi vinavyosababisha ugonjwa wa Ukimwi (VVU), baada ya kuja na dawa kinga zinazoweza kumkinga mtu asiambukizwe virusi hivyo. Wataalamu wa afya wametaja dawa kinga hizo kuwa ni pete kinga inayowekwa ukeni na nyingine ni dawa ya sindano anayochomwa mtu kumkinga ndani ya miezi miwili. Akitoa mafunzo kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mtendaji Mkuu taasisi isiyo ya kiserikali ya DARE Tanzania, Dk. Lilian Mwakyosi, alisema pete kinga ni miongoni mwa njia salama na rahisi kutumia ili kujikinga na VVU hususani kwa wasichana na wanawake kwa…
Na Restuta James NGULI wa nyimbo za injili nchini, Christina Shusho, amesema ‘kituo kinachofuata’ ni tamasha na maonesho ya biashara nchini Dubai, ambayo yatakwenda sambamba na mahubiri ya neno la Mungu. Shusho ameiambia GND jijini Dar es Salaam jana alipokutana na wadau wa maandalizi wa safari ya Dubai kwa wapendwa wanaomiliki biashara. Alisema safari hiyo imeandaliwa na Neema Ministry ya mtumishi wa Mungu, Nabii Neema Sikatenda, wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Alisema safari ya Dubai inajumuisha matukio matano ambayo ni mikutano ya kibiashara, mikutano ya injili, onesho la muziki wa injili, utalii na maonesho ya kibiashara. “Ni tukio muhimu…