Subscribe to Updates
Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.
- EPUKA MAUA HAYA NYUMBANI KWAKO
- FUKUZA NYOKA KWA MIMEA HII
- DARASA LA SABA KUPEWA UFADHILI
- MAENDELEO BENKI YATAJA ONGEZEKO LA FAIDA 2024
- BRELA, UDSM wawanoa wadau faida miliki ubunifu
- Utafiti kilimo, mifugo na uvuvi kutokomeza njaa
- NMB yaja na mwarobaini mikopo kausha damu
- TARI kuzalisha miche 100,000 ya parachichi msimu ujao
Author: Mama Mwenyekiti
SERIKALI ya Norway imeahidi kuendelea kushirikiana na Tanzania kupitia Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA), katika miradi mbalimbali ukiwamo wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Balozi wa Norway nchini, Elisabeth Jacobsen, ameyasema hayo alipotembelea SUA na kuona miradi ya ushiriki wa vijana kwenye kilimo. Amesema kwa zaidi ya miaka 50, Tanzania na Norway zimekuwa na uhusiano mzuri hivyo anakusudia kuendeleza ushirikiano huo kwa kuanzisha na kuendeleza miradi ya kupambana na mabadiliko ya tabianchi hususani hewa ukaa. “Norway pia kuna mambo mengi ya kushirikiana… hatutashiriki kwenye kilimo pekee bali hata kwenye masuala ya miradi ya mabadiliko ya hali ya hewa,” amesema…
RAIS wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa chama cha ACT-Wazalendo, Ikulu mjini Unguja mapema leo. Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Charles Hillary, kwa vyombo vya habari imesema kwamba viongozi hao wamezungumzia ustawi wa Zanzibar kisiasa na kijamii. “Viongozi hao wameafikiana kwamba ipangwe tarehe ya kuzindua rasmi kamati maalumu itakayoundwa na wajumbe kutoka CCM (Chama Cha Mapinduzi) na ACT-Wazalendo, ambavyo ndivyo vilivyounda serikali ya Umoja wa Kitaifa, kuanza kujadiliana na baadae kupanga mpango wa utekelezaji wa ripoti ya kikosi kazi kilichoundwa,” imesema sehemu ya taarifa hiyo. Imefafanua kuwa viongozi wa…
Benki ya NBC imetoa gawio la Sh. bilioni sita kwa Serikali, ikiwa ni sehemu ya faida iliyopatikana mwaka 2022. Akizungumza wakati wa hafla fupi ya makabidhiano ya hundi iliyofanyika leo Mei 17, Jijini Dar es Salaam, Msajili wa Hazina, Nehemia Mchechu, ameipongeza NBC ambayo Serikali ni mmoja ya wanahisa, ikimiliki asilimia 30 ya hisa zake, amesema mafanikio hayo ni matokeo chanya ya utendaji mzuri uliowezesha kupatikana kwa faida nzuri. “Serikali inafurahi kuona uwekezaji wake unakuwa wenye tija. Kiasi cha shilingi bilioni sita tulichopokea leo, kitasaidia katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo,” amesema Mchechu. Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya NBC, Elirehema…
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amezindua mradi wa kuwajengea uwezo Vijana ili Waweze Kujiajiri na Kuajirika katika Sekta ya Uchumi wa Bluu.
TAASISI ya Saratani Ocean Road (ORCI), imetenga siku maalumu ya uchunguzi wa saratani ya ngozi kwa watu wenye ualbino. Taarifa ya ORCI iliyotolewa leo imesema kwamba taasisi hiyo imetenga saa saba kila siku ya Alhamisi kuhudumia kundi hilo la wagonjwa. “Kliniki ya saratani ya ngozi kwa watu wenye ualbino kila Alhamisi kuanzia saa 2:00 hadi saa 9:00 alasiri block A-chumba namba 110,” imesema. Taarifa hiyo imeongeza kuwa: “Karibu upate elimu na uchunguzi wa awali wa saratani…karibuni hata kwa watu wengine wa kawaida.”
MAMLAKA ya Ukanda Maalumu wa Uwekezaji nchini (EPZA), imeita wawekezaji wenye nia ya kuanzisha viwanda ili waendeleze maeneo saba yaliyopo katika mikoa ya Mbeya, Lindi, Dar es Salaam, Tanga na Shinyanga, chini ya utaratibu wa mamlaka hiyo. Taarifa ya Mkurugenzi Mkuu wa EPZA, Charles Itembe, kwa vyombo vya habari imeyataja maeneo yaliyopo Dar es Salaam kuwa ni vitalu namba 184/185 na 186/185 vyenye jumla ya ekari 8.39, zilizopo eneo la viwanda Chang’ombe, katika Manispaa ya Temeke, zilizokuwa zinamilikiwa na iliyokuwa kampuni ya taifa ya chuma. Lingine kwa Dar es Salaam ni mita za mraba 15,000 zilizopo eneo Maalum la Kiuchumi…
SHIRIKA la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO), Mkoa wa Dar es Salaam, limekuja na mkakati wa kusaidia wajasiriamali wadogo kumiliki viwanda baada ya kujenga kituo cha kisasa cha kusindika mazao ya kilimo, chenye huduma muhimu za viwanda vidogo. Meneja wa SIDO, Mkoa wa Dar es Salaam, Ridhiwani Matenge, amesema kituo hicho kinajengwa kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Korea (KOIKA) na kipo mbioni kukamilika. “Ni kituo ambacho kitaweza kutoa mafunzo na uzalishaji kwa wakati mmoja ambapo wajasiriamali watapata mafunzo kwa vitendo na pia itakuwa ni sehemu ya kuzalishia. Jengo hilo likikamilika na kuwekwa vitendea kazi, litakuwa na maeneo sita ya…
TAASISI ya Afya Ifakara (IHI), imeanza kampeni kubwa ya chanjo ya mbwa ili kudhibiti ugonjwa wa kichaa cha mbwa. Kampeni hiyo inafanyika kwa siku 10, kuanzia Jumamosi iliyopita hadi kesho Jumatano. Akizungumza na NIPASHE, kiongozi wa kampeni hiyo kutoka IHI, Dk. Sambo Maganga, amesema kampeni hiyo inafanyika Manispaa ya Tabora Mjini na wanatarajia kuchanja mbwa 15,000 ili kudhibiti ugonjwa huo katika eneo hilo. Kwa mujibu wa taasisi hiyo, ugonjwa wa kichaa cha mbwa husababisha vifo vya watu 552 nchini kwa mwaka huku asilimia 98 waking’atwa na mbwa wa kufugwa.
UGONJWA wa saratani umeendelea kuwa tishio kwa wanawake kutokana na sababu kadhaa ikiwamo kutonyonyesha ipasavyo, kuchelewa kupata mtoto na kutopata chanjo kwa wakati. Takwimu za Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI), za Julai mwaka jana hadi Machi mwaka huu, zinaonyesha kwamba, Tanzania inapata wagonjwa wapya 42,046 kila mwaka na miongoni mwao ni asilimia 44 ya wanawake wanaokabiliwa na saratani ya mlango wa kizazi. Mkurugenzi Mkuu wa ORCI, Dk. Julius Mwaiselage, anasema saratani ya shingo ya kizazi ni tatizo kubwa na imeendelea kuongezeka siku hadi siku. Anasema wanawake walio kwenye hatari ya kupata aina hiyo ya saratani ni wale wenye…
Na Restuta James WANASAYANSI wa Taasisi ya Afya Ifakara (IHI), wanajifungia maabara kwa mwaka mmoja, kutafiti sababu za kuenea kwa ugonjwa sugu wa figo (CKD) na hatari inayowakabili wagonjwa wa tatizo hilo, katika nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara. Utafiti huo uliopewa jina la RenalTWO ni uchunguzi wa kwanza wa muda mrefu juu ya magonjwa sugu ya figo (CKD), ambao umeanza Aprili Mosi, mwaka huu na unatarajiwa kukamilika Machi 31, mwakani. Taarifa iliyotolewa na IHI kwenye tovuti yake, ilieleza kuwa utafiti huo utachunguza matukio ya kuenea kwa CKD, kisukari na shinikizo la damu.