Subscribe to Updates
Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.
- EPUKA MAUA HAYA NYUMBANI KWAKO
- FUKUZA NYOKA KWA MIMEA HII
- DARASA LA SABA KUPEWA UFADHILI
- MAENDELEO BENKI YATAJA ONGEZEKO LA FAIDA 2024
- BRELA, UDSM wawanoa wadau faida miliki ubunifu
- Utafiti kilimo, mifugo na uvuvi kutokomeza njaa
- NMB yaja na mwarobaini mikopo kausha damu
- TARI kuzalisha miche 100,000 ya parachichi msimu ujao
Author: Mama Mwenyekiti
Benki Kuu ya Tanzania (BoT), imejipanga kuwasaidia Wajasiriamali nchini kupitia Mfuko wa Udhamini wa Mikopo kwa ajili ya Mauzo Nje ya Nchi (ECGS), pamoja Mfuko wa Udhamini wa Mikopo kwa Wajasiriamali Wadogo na wa Kati (SME-CGS). Lengo ni kuwezesha wakopaji wenye miradi mizuri, kupata mitaji kutoka kwenye benki na taasisi za fedha, pale wanapokuwa na upungufu wa dhamana ambayo inatoa fursa ya udhamini. Akizungumza katika Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo Nanenane yanayofanyika Nzuguni jijini Dodoma, Mchambuzi Mwandamizi wa Masuala ya Fedha wa BoT, Gloria Samwel Chellunga, amesema benki hiyo inasimamia mfuko wa udhamini wa mkopo kwa niaba ya serikali ili…
Mamlaka ya Maeneo Maalum ya Uwekezaji kwa Mauzo ya Nje (EPZA), imewataka Watanzania kuchangamkia uwekezaji katika maeneo hayo ili wazalishe bidhaa zinazokidhi soko la nje ili kuiongezea nchi fedha za kigeni. Hayo yameelezwa na Kaimu Meneja wa uhamasishaji wa EPZA, Nakadongo Phares, alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo Nane-nane yanayoendelea kwenye viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma. “Tuko hapa Nane-nane kutoa elimu kwa wananchi, lakini pia kuelezea fursa zilizopo za kupata maeneo maalum katika fursa za uwekezaji wa viwanda vinavyozalisha kwa ajili ya kuuza nje ya nchi,” amesema Nakadongo. Amesema EPZA ina programu ya kumwezesha…
Na Mwandishi Wetu Vijana wanaopenda kujiunga na mafunzo ya ufundi wa fani mbalimbali wameitwa na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), kujiunga na vyuo vyake vilivyopo mikoa yote nchini. Tangazo la VETA limetaja baadhi ya fani za ufundi zinaotolewa ni umeme wa magari (AE), mitambo, majokofu na kiyoyozi, ufungaji umeme, msaidizi wa maabara, Sekretarieti na kompyuta, useremala na uunganishaji, teknolojia ya ushonaji na ubunifu wa mavazi na uashi na ufyatuaji matofali. Nyingine ni ujenzi na matengenezo ya barabara, uchoraji na uandishi wa alama, uchomeleaji na utengenezaji wa vyuma, teknolojia ya usindikaji wa nyama, mapishi, huduma za chakula…
WANAWAKE, Vijana na wenye mahitaji maalumu wameshauriwa kujiunga na mfumo wa manunuzi ya umma (National e-Procurement System of Tanzania-NeST), ili waweze kuona zabuni za umma mara tu zinapotangazwa na kuziomba. Akizungumza kwenye mkutano wa asubuhi (breakfast meeting), ulioandaliwa na Chemba ya Wanawake Wafanyabiashara Tanzania (TWCC), na kuwakutanisha wanawake na vijana zaidi ya 300, Meneja wa Mamlaka ya Usimamizi wa Manunuzi ya Umma (PPRA), Kanda ya Pwani, Vicky Mollel, amesema wanawake wana nafasi ya kukuza biashara zao kupitia miradi ya serikali kwa njia ya zabuni. Amesema ili kushinda zabuni, ni muhimu kwa wanawake kujisajili kwenye mfumo wa NeST, ili watambulike na…
WANANCHI 75,000 wamefikiwa na programu ya Imarisha Uchumi na Mama Samia (IMASA), katika mikoa nane, wengi wao wakiwa ni wanawake na vijana. Akizungumza na BUSTANI jijini Dar es Salaam hivi karibuni, Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji wananchi kiuchumi (NEEC), Beng’i Issa, amesema lengo la mpango huo ni kuimarisha uchumi wa vijana, wanawake, watu wenye ulemavu pamoja na wazee, ambao tayari wanafanya biashara ndogo ndogo kwenye vikundi au mmoja mmoja.
Na Mwandishi Wetu, Morogoro WAKALA wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), umetahadharisha matumizi ya ‘vishoka’ kusajili kampuni, huduma au majina ya biashara, kwa kuwa wengi hutumia taarifa za wahusika vibaya. Akiwasilisha mada kwenye mafunzo ya waandishi wa habari za biashara yanayofanyika mjini hapa, Meneja katika sehemu ya makampuni BRELA, Lameck Nyangi, amesema huduma za taasisi hiyo zinapatikana kwa urahisi kwa njia ya mtandao (ORS), ambao unamlazimu mhusika kujisajili kwa jina lake ili aweze kuhudumiwa. “Unakuta mtu anarahisisha tu mambo, anamtafuta mtu anamwambia amsajilie kampuni hadi anampa taarifa zake muhimu wala hajishughulishi kujua ni namna gani mfumo unafanyakazi, matokeo yake…
Na Restuta James FAMILIA nyingi kama sio zote zenye uwezo wa kununua televisheni au radio wanazo. Nyumba hizo hizo, ni chache au chini ya nusu hazina maktaba walau ya vitabu vichache. Hali hii imejenga tabia ya wanafamilia na hasa watoto kupenda kuangalia na kusikiliza vipindi zaidi badala ya kusoma. Kama wewe ni mzazi au mlezi nakuletea mbinu ya kuanzisha maktaba ndogo nyumbani ili watoto wanufaike na maarifa mengi yaliyofichwa vitabuni. Walimu wa watoto wadogo wanaeleza kuwa mtoto mwenye umri kuanzia miaka miwili na nusu wanauwezo wa kujifunza kusoma na wakajua ndani ya muda mfupi, kama mazingira wenzeshi wataanzia nyumbani. Wanashauri…
Na Restuta James UKISASA wa vitu vingi duniani unahamia kwenye kuboresha vitu vya asili kuanzia aina ya ujenzi wa nyumba hadi mapambo yake. Leo tunaangazia mapambo ya ndani yanayotokana na vitu asilia kama ukili, katani, migomba na kamba za aina mbalimbali ambazo miongo kadhaa iliyopita zilionekana kama vitu vya watu masikini. Kama inavyoonekana pichani, ubunifu wa kazi za mikono zilizonakishiwa kwa rangi ni pambo la nyumba za ‘matajiri’ ndani na nje ya Afrika. Wataalamu wa mapambo ya ndani wanaeleza kuwa sanaa ya ubunifu ndio inaosababisha kazi za mikono kuteka soko la kimataifa la urembo na mapambo. Anastazia Jonathan, anasema upambaji…
Na Mwandishi Wetu, Morogoro WAKALA wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), umesema matumizi ya teknlojia kupata huduma zinazotolewa na taasisi hiyo yameondoa urasimu na kuwawezesha wananchi kupata leseni katika kipindi cha siku moja hadi tatu za kazi. Akizungumza kwenye mafunzo ya waandishi wa habari mjini hapa leo Juni 18, 2024; Mkurugenzi wa Leseni BRELA, Andrew Mkapa, amesema maboresho ya wakala huo ambayo yamewaruhudu wafanyabiashara kujisajili kwa mfumo wa mtandao (online), yanalenga kupunguza muda wa kupata huduma hadi siku moja. “Tunataka kama mfanyabiashara atakuwa amekamilisha vielelezo vyote muhimu kama namba ya mtambulisho wa mlipa kodi, kitambulisho cha taifa, vibali vya…
Na Restuta James, Morogoro KATIBU Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dk. Hashil Abdalllah, amewahimiza waandishi wa habari kuelimisha umma umuhimu wa kurasimisha biashara, ili waweze kunufaika na fursa zitakazowawezesha kukuza mapato. Dk. Hashil ameyasema hayo leo Juni 18, 2024, mjini Morogoro alipokuwa akifungua mafunzo ya waandishi wa habari wanaoripoti kutoka jiji la Dar es Salaam. Amesema kupitia vyombo vya habari, umma unaweza kupata taarifa muhimu kwa haraka na kwa wakati, ikiwemo namna ambavyo wananchi wanaweza kutumia mabadiliko na ukuaji wa teknolojia, kurasimisha biashara kupitia kwa Wakala wa usajili wa biashara na leseni (BRELA). “Niwaombe ndugu zangu wanahabari, kupitia…