Subscribe to Updates
Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.
- EPUKA MAUA HAYA NYUMBANI KWAKO
- FUKUZA NYOKA KWA MIMEA HII
- DARASA LA SABA KUPEWA UFADHILI
- MAENDELEO BENKI YATAJA ONGEZEKO LA FAIDA 2024
- BRELA, UDSM wawanoa wadau faida miliki ubunifu
- Utafiti kilimo, mifugo na uvuvi kutokomeza njaa
- NMB yaja na mwarobaini mikopo kausha damu
- TARI kuzalisha miche 100,000 ya parachichi msimu ujao
Author: Mama Mwenyekiti
Benki Kuu ya Tanzania imetoa mwongozo kwa wakopeshaji wa kidigitali na kupiga marufuku wakopeshaji mtandaoni kutumia lugha za kudhalilisha, kuchapisha taarifa za waliokopeshwa mtandaoni au kutuma jumbe kwenye namba zilizopo katika simu ya aliyekopeshwa. Muongozo wa Agosti 2024, unakuja wakati ambao kuna ongezeko la taasisi mbalimbali zinazotengeneza App za kukopesha; ambazo baadhi zinalalamikiwa kwa utendaji usiofaa. Mathalani tarehe 04 Juni 2024, baadhi ya wabunge walilamika kuhusu kuungwa kwenye makundi ya WhatsApp ambapo vitambulisho vya watu wanaosemwa kuwa na madeni vimekuwa vikitumwa, huku pia wakituma jumbe fupi kwa namba za watu wa karibu wa waliokopeshwa. Mwongozo huo wa BoT, unataka mkopeshaji…
Wajasiriamali katika Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa, vimenufaika na mtaji wezeshi wa Sh. 101.6 milioni kutoka benki ya CRDB, kwa ajili ya kuimarisha biashara zao. Hafla ya kukabidhi hundi hiyo imefanyika jana Septemba 18, kwa vikundi nane na kutoa semina ya kuvijengea uwezo vikundi vya wanawake wajasiriamali na vijana wanufaika wa programu ya Imbeju. Waziri wa Maliasili na Utalii ambaye pia ni mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Njombe, Dk. Pindi Chana, alifungua mafunzo hayo na kuwataka wanufaika kuitumia fursa zinazotolewa na CRDB kukuza ujasiriamali. Waziri Chana amesema fursa waliyopata ni mwendelezo wa juhudi za Serikali katika kuboresha biashara za…
Wakulima na maofisa ugani kutoka Kata 31 za Muheza-Tanga na Hai na Siha-Kilimanjaro, wamepewa mbinu za kudhibiti wadudu waharibifu wa matunda aina ya parachichi, machungwa na embe, ili kilimo hicho kiwaletee manufaa stahiki. Mafunzo hayo yametolewa na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI), kupitia vituo vyake vya Ukiriguru (Mwanza), Tengeru (Arusha) na Mlingano (Tanga), kwa kushirikiana na watafiti kutoka Kituo cha Kimataifa cha Utafiti wa Fiziolojia na Ikolojia ya Wadudu (ICIPE), cha Nairobi nchini Kenya. Watafiti waliwanoa wakulima na maofisa ugani hao katika mafunzo ya siku tano, ikiwa ni utekelezaji wa mradi wa njia husishi za kudhibiti wadudu wa…
WAJASIRIAMALI nchini wametakiwa kuzalisha bidhaa zenye ubora ili waweze kushindana katika soko la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Afrika na mabara mengine. Aidha, mashirika ya viwango ya nchi za EAC yameingia makubaliano, ambapo bidhaa ikishathibitishwa ubora na shirika la viwango la nchi husika, haitakiwi kupimwa tena inapopelekwa kwenye soko la nchi nyingine. Wito huo ulitolewa mwishoni mwa wiki na Ofisa Uthibiti Ubora wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Sileja Lushibika, wakati akitoa elimu kwa wajasiriamali 46 pamoja na wananchi kwenye maonesho ya saba ya mifuko ya programu za kuwawezesha wananchi kiuchumi. Maonesho hayo yalifanyika mkoani Singida katika Viwanja vya Bombadier…
Waziri wa Viwanda na Biashara, Selemani Jafo, amewataka wabunifu wote nchini kulinda bunifu zao kwa kuzisajili kisheria, ili zisichukuliwe na watu wengine na kujinufaisha nazo bila kufuata utaratibu wa kisheria. Ametoa wito huo wakati wa ziara aliyoifanya ofisi za Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), jijini Dar es Salaam ili kujionea utendaji kazi na kujifunza namna wakala inavyotoa huduma. Amesema kuna bunifu nyingi ambazo zinachukuliwa na watu wengine wanaziendeleza na kujiongezea kipato, bila wabunifu waanzilishi kunufaika na chochote kwa kuwa hawakuzisajili. “Ninatoa wito kwa Watanzania wabunifu wote kusajili bunifu zenu kupitia BRELA, maana taasisi hii inakazi ya kulinda…
VIJANA 10 wa Kitanzania wameula kwa kupata ufadhili wa Sh. 250 milioni, kutoka Wizara ya Nishati kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo (UNDP), Umoja wa Ulaya (EU) na Ubalozi wa Ireland, ili kuendeleza bunifu zao zinazolenga kuboresha upatikanaji wa nishati safi nchini. Wabunifu hao 10 ni sehemu ya 159 waliowasilisha mawazo bunifu na kufanyiwa mchujo na wataalamu wa masuala ya nishati. Naibu Kamishna wa Nishati Jadidifu kutoka Wizara ya Nishati, Imani Mruma, amesema lengo la kuanzishwa mchakato wa kufadili bunifu kwenye nishati ni kuchochea maendeleo ya suluhisho na teknolojia za msingi zenye uwezo wa…
Mkurugenzi Mtendaji wa Chemba ya Wafanyabiashara Wanawake Tanzania (TWCC), Mwajuma Hamza, amewataka wanawake na vijana kuchangamkia fursa ya Eneo Huru la Biashara la Afrika (AfCFTA), ili wakuze haraka biashara zao. Ameyasema hayo mkoani Kagera alipokuwa akifungua mafunzo ya taratibu, kanuni na sheria za kufanya biashara katika eneo hilo, yaliyoandaliwa na TWCC kwa kushirikiana na Trade Mark Africa. Alisema soko hilo linakadiriwa kuwa na watu bilioni 1.3 na kwamba programu nyingine inayotekelezwa na chemba hiyo ni ile ya zabuni (Bid for Success-B4S). “Kiu yetu ni kuona wanawake na vijana wanafika masoko makubwa, wanapata zabuni za serikali na binafsi na kwenye miradi…
WANAWAKE na vijana wameanza kupigwa msasa ili waweze kushiriki zabuni za umma na binafsi, kwa kupewa mbinu za kuandaa nyaraka zinazokidhi taratibu za kisheria wakati wa mchakato wa kuomba kazi au kutoa huduma kwenye taasisi mbalimbali. Wanawake na vijana 30 wameanza mafunzo hayo katika awamu ya kwanza jijini Dar es Salaam na yanatolewa na Chemba ya Wafanyabiashara Wanawake Tanzania (TWCC), kwa ufadhili wa TradeMark Africa. Akifungua mafunzo hayo leo, Mkurugenzi Mtendaji wa TWCC, Mwajuma Hamza, amesema: “Tunategemea kuwafikia takribani wanawake na vijana 400 ndani ya miaka mitatu na katika kundi la kwanza tumeanza na 30. Watejengewa uelewa wa kina kuhusu…
Kampuni ya PASS Trust kwa kushirikiana na Benki ya Equity Tanzania wameingia mkataba wa kuwawezesha wajasiriamali walio kwenye mnyororo wa kuongeza thamani mazao ya kilimo, ufugaji, uvuvi, mazao ya misitu na viwanda. Wamesaini mkataba wa kuendeleza uhusiano wa kibiashara mbele ya Naibu Waziri wa Kilimo, David Silinde na kuratibiwa na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara wa PASS Trust, Adam Kamanda pamoja na Meneja Mkuu wa Biashara wa Equity Benki, Leah Ayoub katika Maonesho ya wakulima, wafugaji na wavuvi (Nane Nane – 2024) yanayofanyika katika viwanja vya Nane Nane jijini Dodoma. Mkataba uliosainiwa unalenga kuwafikia zaidi wakulima wadogo na wa kati…
Benki Kuu ya Tanzania (BoT), imesema itaendelea kutengeneza mazingira rafiki kwa wakulima ili waweze kupata mikopo kwa riba nafuu itakayowasaidia kufikia malengo na kupiga hatua ya maendeleo. Akizungumza kwenye mahojiano katika Maonesho ya kimataifa ya kilimo Nanenane yanayofanyika Nzuguni jijini Dodoma, Afisa Mkuu Mwandamizi, Kurugenzi ya Usimamizi Sekta ya Fedha, Idara ya huduma ndogo ya Fedha, BoT, Deogratius Mnyamani, amesema BoT imetenga fedha kwa ajili ya taasisi za fedha zikiwamo benki ili waweze kuwakopesha wakuilimo kwa riba nafuu. Amesema lengo ni kuhakikisha wakulima wanapata mikopo kwa gharama nafuu ili kuleta tija kwa Taifa katika sekta ya kilimo. Amesema ili mkulima…